Jeremiah 4:19-21


19 aEe mtima wangu, mtima wangu!
Ninagaagaa kwa maumivu.
Ee maumivu makuu ya moyo wangu!
Moyo wangu umefadhaika ndani yangu,
siwezi kunyamaza.
Kwa sababu nimesikia sauti ya tarumbeta,
nimesikia kelele ya vita.

20 bMaafa baada ya maafa,
nchi yote imekuwa magofu.
Kwa ghafula mahema yangu yameangamizwa,
makazi yangu kwa muda mfupi.

21 cHata lini nitaendelea kuona bendera ya vita
na kusikia sauti za tarumbeta?

Copyright information for SwhKC